Friday, April 13, 2012

women of courage Award 2012-Joaquine De-Mello atunukiwa Tuzo ya Mwanamke Jasiri Tanzania 2012

Ofisa wa Mambo ya Nje wa Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania, Dana Banks akizungumza wakati wa hafla ya kumtunuku Tuzo ya Mwanamke Jasiri Tanzania 2012, Bi. Joaquine De-Mello iliyofanyika katika ubalozi huo jijini Dar es Salaam leo Machi 29.12. De-Mello ni Mwanasheria Kitaaluma na amekuwa Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora tangu Mwaka 2008. Aidha Ubalozi wa Marekani hapa Nchini umeamua kumtunuku tuzo hiyo kutokana na juhudi zake za kutetea Haki za Wanawake hapa nchini. PICHA ZOTE/JOHN BADI

De-Mello akiwa katika picha ya pamoja na Robert Scott na Dana Banks
Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Alice Foundation ambaye pia ni Mkurugenzi wa Alice Fashion World, Alice James Dosi akikabidhi zawadi ya maua kwa De-Mello kama ishara ya kumpongeza.